JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA FEDHA

BARAZA LA MASOKO YA MITAJI

Majukumu

Jukumu la msingi la Baraza ni kusuluhisha migogoro na mgawanyiko inayojitokeza katika utekelezaji wa Sheria ya Masoko ya Mitaji na Dhamana Sura ya 79, hususan kwenye tafsiri ya sheria au kanuni zinazotumika chini ya Sheria hiyo, kati ya washiriki wa masoko. Baraza katika utekelezaji wa jukumu lake itahakikisha kwamba maamuzi yanatolewa kwa misingi ya haki na kwa uharaka ili kila washiriki wa soko wanatekeleza wajibu wao kwa mujibu wa Sheria. Hii ikiwa ni pamoja na kuboreshaji wa utatuzi wa migogoro ya masoko ya mitaji yanayojitokeza kulingana na Sheria, kwa lengo la kukuza uadilifu katika masoko. Hata hivyo, katika utekelezaji wa jukumu lake la msingi, Baraza haitakuwa na mamlaka ya kushughulikia makosa ya jinai.