NYARAKA ZA RUFAA
NYARAKA MUHIMU
NYARAKA MUHIMU ZITAKAZO AMBATISHWA KWENYE RUFAA
Mtu anayekata rufaa kwa Baraza ataambatisha nyaraka zifuatazo:
- Nakala iliyothibitishwa ya uamuzi wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana.
- Nakala ya taarifa ya nia ya kukata rufaa.
- Maelezo ya rufaa.
- Nyaraka nyingine muhimu ambazo mkata rufaa anaweza kuziona zinahitajika kwa ajili ya maamuzi sahihi ya rufaa hiyo.
- Ushahidi wa malipo ya ada husika.